#Geneva : Ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa imesema kwamba ongezeko la joto duniani lilifikia viwango vya rekodi mwaka 2025. Miaka 10 yenye joto kali zaidi kuwahi kurekodiwa yote ilikuwa kati ya 2015 na 2025, shirika la hali ya hewa na tabianchi la Umoja wa Mataifa , WMO, lilithibitisha katika ripoti yake kuu ya mwaka ya Hali ya Tabianchi Duniani. Mwaka jana ulikuwa mwaka wa pili au wa tatu kuwa na joto kali zaidi kuwahi kurekodiwa, ukiwa takriban nyuzijoto 1.43 kwenye vipimo vya Selsiasi. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema kuwa kila kiashiria muhimu cha mabadiliko ya tabianchi kinaonyesha hatari nyekundu. #dwhabari #dwkiswahili #Mazingira #tabianchi